SIRI ZA BIBLIA: MWANADAMU WA KWANZA KUZALIWA NA KUUA-KAINI
Manage episode 313499888 series 3273506
Kaini kadiri ya Biblia ni jina la binadamu wa kwanza kuzaliwa na kuua.
Kadiri ya kitabu cha Mwanzo (Biblia) katika Agano la Kale wana wawili wa kwanza wa Adamu na Hawa, majina yao Kaini na Habili, walitunza imani yao kwa Mungu wakamtolea sadaka.
Habili aliitoa katika wanyama bora wa kundi lake, akiwa na hali ya unyenyekevu na imani, naye Mungu akampokea.
Tabia ya Kaini ilikuwa ya kiburi, bila ya kumcha Mungu, kwa hiyo Mungu alimkataa (4:1-5; taz. Ebr 11:4; 1 Yoh 3:12).
Tabia na maisha ya watoaji wa sadaka ina maana kuliko vitu wanavyovitoa, kwa hiyo Mungu alimwambia Kaini kuwa, akitaka Mungu ampokee, angepaswa kushinda dhambi iliyokuwa ikitaka kumwangamiza. Dhambi hiyo ilikuwa kama mnyama wa mwitu ajikunjaye na kuotea mlangoni, ili aweze kumshambulia mtu akitoka nje (4:6-7).
Kaini hakushinda dhambi yake, na katika hasira ya wivu alimwua Habili. Tendo lake la kutwaa uzima wa ndugu yake lilidai kisasi kwa Mungu aliyetoa uhai ule. Kwa hiyo Mungu alimfukuza Kaini aende mbali na mahali walipoishi watu wengine.
Ingawa Kaini alidumu katika hali ya kutotubu, Mungu katika huruma yake kubwa alimlinda asiuawe kwa kisasi (4:8-16).
--- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/siri-za-biblia/message119 episodes