Artwork

Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Player FM - Podcast App
Go offline with the Player FM app!

Maelfu ya wapalestina washikiliwa na mamlaka za Israeli bila kujulikana waliko

1:57
 
Share
 

Manage episode 431719663 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Hii leo ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, OHCHR, imechapisha ripoti kuhusu mamlaka za Israeli kukamata wapalestina kiholela na kwa muda mrefu tangu mwezi Oktoba mwaka jana akiwemo mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 80 mwenye ugonjwa wa kusahau. Assumpta Massoi amepitia ripoti hiyo na kuandaa taarifa ifuatayo. (Taarifa ya Assumpta Massoi)Ripoti ni ya kurasa 23 ikiweka bayana machungu wanayopitia wale wanaoshikiliwa na Israeli, halikadhalika ikinyooshea mkono vikundi vilivyojihami vya kipalestina, ikiwemo Hamas ambao wanashikilia mateka wa Israeli tangu vita ianze Oktoba 7 mwaka jana.Wapalestina walikamatwa wakati wamesaka hifadhi kwenye shule, hospitail, nyumbani au kwenye vituo vya ukaguzi wakati idadi kubwa ya wapalestina walikuwa wanahama kutoka kaskazini mwa Gaza kuelekea kusini.Miongoni mwao ni mwanamke huyo wa umri wa zaidi ya miaka 80 pamoja na wasichana, wavulana, na wanaume wasiohusiana na vikundi vilivyojihami.Jeremy Laurence, Msemaji wa Ofisi hiyo ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu anasema, ripoti inajumuisha madai ya kuteswa na kutendewa vibaya na aina nyingine za ukatili. Mahabusu wanashikiliwa kwenye maeneo kama vizimba, wanavuliwa nguo zote na kuachwa na nguo ya ndani pekee kwa muda mrefu, mbwa wakiachiliwa wawang’ate, wananing’inizwa kwenye dari na pia kuna ripoti za ukatili wa kijinsia na kingono wanapokuwa wanashikiliwa.”Mamlaka za Palestina kwa upande wake zimeripotiwa kukamata kiholela watu huko Ukingo wa Magharibi ili kuzuia kukosolewa na upinzani wa kisiasa.Bwana Laurence anasema sheria ya kimataifa inataka wale wanaoshikiliwa watendewe kiutu na kibinadamu na inakataza mateso au aina nyingine ya ukatili.Hivyo anasema, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu. Volker Türk, anasisitiza wito wake wa kuachiliwa mara moja kwa mateka wote wanaoshikiliwa Gaza. Wapalestina wote wanaoshikiliwa kiholela na Israeli lazima waachiliwe huru.Kamishna Mkuu Türk ametaka pia uchunguzi wa haraka, huru na wa kina wa matukio yote yaliyosababisha ukiukwaji wa sheria ya kimataifa, na kuhakikisha wahusika wanawajibishwa na kwamba manusura na familia zao wapatiwe haki yao ya fidia. TAGS: Haki za binadamuAdditional: Amani na UsalamaNews: Gaza, Palestina, IsraeliRegion: Mashariki ya KatiUN/Partner: OHCHR
  continue reading

104 episodes

Artwork
iconShare
 
Manage episode 431719663 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Hii leo ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, OHCHR, imechapisha ripoti kuhusu mamlaka za Israeli kukamata wapalestina kiholela na kwa muda mrefu tangu mwezi Oktoba mwaka jana akiwemo mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 80 mwenye ugonjwa wa kusahau. Assumpta Massoi amepitia ripoti hiyo na kuandaa taarifa ifuatayo. (Taarifa ya Assumpta Massoi)Ripoti ni ya kurasa 23 ikiweka bayana machungu wanayopitia wale wanaoshikiliwa na Israeli, halikadhalika ikinyooshea mkono vikundi vilivyojihami vya kipalestina, ikiwemo Hamas ambao wanashikilia mateka wa Israeli tangu vita ianze Oktoba 7 mwaka jana.Wapalestina walikamatwa wakati wamesaka hifadhi kwenye shule, hospitail, nyumbani au kwenye vituo vya ukaguzi wakati idadi kubwa ya wapalestina walikuwa wanahama kutoka kaskazini mwa Gaza kuelekea kusini.Miongoni mwao ni mwanamke huyo wa umri wa zaidi ya miaka 80 pamoja na wasichana, wavulana, na wanaume wasiohusiana na vikundi vilivyojihami.Jeremy Laurence, Msemaji wa Ofisi hiyo ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu anasema, ripoti inajumuisha madai ya kuteswa na kutendewa vibaya na aina nyingine za ukatili. Mahabusu wanashikiliwa kwenye maeneo kama vizimba, wanavuliwa nguo zote na kuachwa na nguo ya ndani pekee kwa muda mrefu, mbwa wakiachiliwa wawang’ate, wananing’inizwa kwenye dari na pia kuna ripoti za ukatili wa kijinsia na kingono wanapokuwa wanashikiliwa.”Mamlaka za Palestina kwa upande wake zimeripotiwa kukamata kiholela watu huko Ukingo wa Magharibi ili kuzuia kukosolewa na upinzani wa kisiasa.Bwana Laurence anasema sheria ya kimataifa inataka wale wanaoshikiliwa watendewe kiutu na kibinadamu na inakataza mateso au aina nyingine ya ukatili.Hivyo anasema, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu. Volker Türk, anasisitiza wito wake wa kuachiliwa mara moja kwa mateka wote wanaoshikiliwa Gaza. Wapalestina wote wanaoshikiliwa kiholela na Israeli lazima waachiliwe huru.Kamishna Mkuu Türk ametaka pia uchunguzi wa haraka, huru na wa kina wa matukio yote yaliyosababisha ukiukwaji wa sheria ya kimataifa, na kuhakikisha wahusika wanawajibishwa na kwamba manusura na familia zao wapatiwe haki yao ya fidia. TAGS: Haki za binadamuAdditional: Amani na UsalamaNews: Gaza, Palestina, IsraeliRegion: Mashariki ya KatiUN/Partner: OHCHR
  continue reading

104 episodes

All episodes

×
 
Loading …

Welcome to Player FM!

Player FM is scanning the web for high-quality podcasts for you to enjoy right now. It's the best podcast app and works on Android, iPhone, and the web. Signup to sync subscriptions across devices.

 

Quick Reference Guide