29 AGOSTI 2024
MP3•Episode home
Manage episode 436917033 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Yaliyomo kwenye Jarida la Habari za UN hii leo ni pamoja na ziara ya Katibu Mkuu wa UN huko Timor-Leste; maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kupinga majaribio ya nyuklia na kauli ya Mkurugenzi Mteule wa WHO kanda ya Afrika, Dkt. Faustine Ndugulile baada ya kuteuliwa. Mada kwa kina ni Morogoro Tanzania. Na pia kuna kujifunza lugha ya kiswahili. Karibu na mwenyeji wako ni Anold Kayanda.Nchini Tanzania katika mkoa wa Morogoro, ulioko mashariki mwa nchi hiyo, wakulima 50 kutoka skimu za umwagiliaji za Ifakara Dakawa mkoani humo na Mbarali mkoa wa Mbeya, kusini magharibi mwa Tanzania wamepatiwa ujuzi wa kutumia zana bora za kisasa za Kilimo cha mpunga ikiwemo zana za kusawazisha mashamba, kupanda mbegu na kuvuna. Lengo ni kuongeza thamani katika uzalishaji wa zao la mpunga. Mafunzo yaliyotolewa na Taasisis ya Utafiti wa Kilimo TARI kwa usimamizi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO huku zana zikiwezeshwa na shirika la Korea Kusini la ushirikiano wa maendeleo, KOICA. Hamad Rashid wa Redio washirika Tanzania Kids Time FM mkoani Morogoro alifika kwenye skimu hiyo kuzungumza na wakulima walionufaika. Je wajua neno la kiingereza LINK tafsiri yake ni ipi kwa lugha ya Kiswahili? Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania anafafanua.
…
continue reading
101 episodes