Artwork

Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Player FM - Podcast App
Go offline with the Player FM app!

Madaraja yaliyojengwa na UNMISS yaondolea adha wananchi nchini Sudan Kusini

2:04
 
Share
 

Manage episode 430563851 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini (UNMISS) umefadhili ujenzi wa madaraja matatu huko Yubu, Turbiwa na Bundri kwenye kaunti ya Tambura jimboni Equitoria Magharibi. Lengo la ujenzi huo kupitia miradi ya matokeo ya haraka au QIPs, ni kurahisisha kurudi nyumbani kwa hiari kwa wakimbizi waliofurushwa makwao.Madaraja hayo matatu yanalenga kuwaunganisha watu, kuimarisha mshikamano wa kijamii, na kuboresha upatikanaji wa huduma za afya, shule, na masoko halikadhalika utekelezaji wa jukumu la ulinzi wa raia.Benina Mbiko, mama wa watoto watano, anaamini kwamba daraja hilo litaongeza biashara na hivyo kuinua uchumi na zaidi ya yote..."Kwetu sisi tulio kijijini, huwa ni vigumu kuja mjini wakati wa msimu wa mvua kwa sababu maji yanapokuwa mengi, hatuwezi kuvuka mto. Daraja hili ni zuri sana, asante kwa wale waliojitokeza kutujengea." Kwa wengi, miundombinu mipya inayonufaisha jamii nzima ni ishara ya maendeleo yanayokuwa kama anavyoeleza Chifu Mkuu wa Kijiji cha Tambura, Mboribamo Renzi.Anasema daraja hili litasaidia jamii kwa jumla katika nyanja za kilimo, kusafirisha bidhaa zao hadi sokoni, kurahisisha usafiri wa wagonjwa kutoka vijijini hadi mjini, kuimarisha usalama; na haya yote ni sehemu ya maendeleo.”Kwa upande wake, Mwakilishi wa UNMISS, Anthony Moudie, alisisitiza athari chanya za mradi kama huu akisema..‘‘Daraja hili litasaidia au kurahisisha ulinzi wa raia wa pande zote mbili. Litasaidia serikali kupeleka vyombo vya usalama kuhakikisha kuwa raia wanakuwa salama. Pia, daraja hili litafanikisha upatikanaji wa misaada ya kibinadamu kwa pande zote mbili.’’UNMISS imesema itaendelea kufadhili baadhi ya miradi midogo inayodhaniwa kuwa na uwezo wa kuboresha kwa kiasi kikubwa maisha ya jamii za maeneo ambako miradi hiyo inatekelezwa.
  continue reading

106 episodes

Artwork
iconShare
 
Manage episode 430563851 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini (UNMISS) umefadhili ujenzi wa madaraja matatu huko Yubu, Turbiwa na Bundri kwenye kaunti ya Tambura jimboni Equitoria Magharibi. Lengo la ujenzi huo kupitia miradi ya matokeo ya haraka au QIPs, ni kurahisisha kurudi nyumbani kwa hiari kwa wakimbizi waliofurushwa makwao.Madaraja hayo matatu yanalenga kuwaunganisha watu, kuimarisha mshikamano wa kijamii, na kuboresha upatikanaji wa huduma za afya, shule, na masoko halikadhalika utekelezaji wa jukumu la ulinzi wa raia.Benina Mbiko, mama wa watoto watano, anaamini kwamba daraja hilo litaongeza biashara na hivyo kuinua uchumi na zaidi ya yote..."Kwetu sisi tulio kijijini, huwa ni vigumu kuja mjini wakati wa msimu wa mvua kwa sababu maji yanapokuwa mengi, hatuwezi kuvuka mto. Daraja hili ni zuri sana, asante kwa wale waliojitokeza kutujengea." Kwa wengi, miundombinu mipya inayonufaisha jamii nzima ni ishara ya maendeleo yanayokuwa kama anavyoeleza Chifu Mkuu wa Kijiji cha Tambura, Mboribamo Renzi.Anasema daraja hili litasaidia jamii kwa jumla katika nyanja za kilimo, kusafirisha bidhaa zao hadi sokoni, kurahisisha usafiri wa wagonjwa kutoka vijijini hadi mjini, kuimarisha usalama; na haya yote ni sehemu ya maendeleo.”Kwa upande wake, Mwakilishi wa UNMISS, Anthony Moudie, alisisitiza athari chanya za mradi kama huu akisema..‘‘Daraja hili litasaidia au kurahisisha ulinzi wa raia wa pande zote mbili. Litasaidia serikali kupeleka vyombo vya usalama kuhakikisha kuwa raia wanakuwa salama. Pia, daraja hili litafanikisha upatikanaji wa misaada ya kibinadamu kwa pande zote mbili.’’UNMISS imesema itaendelea kufadhili baadhi ya miradi midogo inayodhaniwa kuwa na uwezo wa kuboresha kwa kiasi kikubwa maisha ya jamii za maeneo ambako miradi hiyo inatekelezwa.
  continue reading

106 episodes

Усі епізоди

×
 
Loading …

Welcome to Player FM!

Player FM is scanning the web for high-quality podcasts for you to enjoy right now. It's the best podcast app and works on Android, iPhone, and the web. Signup to sync subscriptions across devices.

 

Quick Reference Guide