Artwork

Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Player FM - Podcast App
Go offline with the Player FM app!

Polio yathibitishwa Gaza, WHO yasema ni mtoto mwenye umri wa miezi 10

2:02
 
Share
 

Manage episode 435781655 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Vuta nikuvute ikiendelea Gaza kuhusu ufikishaji, usambazaji na utoaji wa chanjo dhidi ya polio wakati huu ambapo makombora yanaendelea kurindima kutoka jeshi la Israeli, hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO, limethibitisha kubainika kwa mgonjwa mmoja wa polio, ikiwa ni miaka 25 tangu ugonjwa huo utokomezwe eneo hilo. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.(Taarifa ya Assumpta Massoi)Ni kwamba tarehe 20 mwezi uliopita wa Julai, mtoto huyo mwenye umri wa miezi 10 alilazwa katika hospitali ya Al-Aqsa akiwa ana homa kali, anatapika, anahara huku akiwa hana nguvu mwilini, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA katika ripoti yake ya 130 kutolewa tangu vita ianze huko Gaza, ikimulika Gaza, Ukingo wa Magharibi na Yerusalem Mashariki.Tarehe 22 Wizara ya Afya kwenye eneo linalokaliwa la Palestina likathibitisha ugonjwa wa polio virusi namba 2 kwa mtoto huyo ambaye hakuwa amepatiwa chanjo kutoka Deir al-Balah huko Gaza. Siku tatu baadaye yaani tarehe 25 Julai mtoto huyo akapooza sehemu ya chini ya mguu wake. Hivi sasa anaendelea na matibabu na hali yake ni nzuri.Uchunguzi uliofanywa na Kituo cha Marekani cha Kudhibiti na Kuzuia magonjwa, CDC ukaunganisha virusi hivyo na aina ya ile iliyobainika kwenye mazingira huko Gaza mwezi Juni mwaka huu.Sasa WHO imethibitisha kuwa ni polio ambapo Mkurugenzi Mkuu wa UNRWA Philippe Lazzarini kupitia mtandao wa X amesema “inasikitisha sana kwamba mtoto huyo amepooza kutokana na Polio. Polio haitotofautisha kati ya watoto wa Palestina na Israeli. Kuchelewecha sitisho la mapigano kwa misingi ya kiutu kutaongeza hatari ya ugonjwa huo kusambaa zaidi kwa watoto.”Awamu mbili za utoaji chanjo zimepangwa kuanza wiki zijazo na UNRWA imesema wataalamu wake wa afya na kupitia kliniki zake tembezi watasaidia usambazaji kwa ushirikiano na WHO na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.
  continue reading

101 episodes

Artwork
iconShare
 
Manage episode 435781655 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Vuta nikuvute ikiendelea Gaza kuhusu ufikishaji, usambazaji na utoaji wa chanjo dhidi ya polio wakati huu ambapo makombora yanaendelea kurindima kutoka jeshi la Israeli, hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO, limethibitisha kubainika kwa mgonjwa mmoja wa polio, ikiwa ni miaka 25 tangu ugonjwa huo utokomezwe eneo hilo. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.(Taarifa ya Assumpta Massoi)Ni kwamba tarehe 20 mwezi uliopita wa Julai, mtoto huyo mwenye umri wa miezi 10 alilazwa katika hospitali ya Al-Aqsa akiwa ana homa kali, anatapika, anahara huku akiwa hana nguvu mwilini, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA katika ripoti yake ya 130 kutolewa tangu vita ianze huko Gaza, ikimulika Gaza, Ukingo wa Magharibi na Yerusalem Mashariki.Tarehe 22 Wizara ya Afya kwenye eneo linalokaliwa la Palestina likathibitisha ugonjwa wa polio virusi namba 2 kwa mtoto huyo ambaye hakuwa amepatiwa chanjo kutoka Deir al-Balah huko Gaza. Siku tatu baadaye yaani tarehe 25 Julai mtoto huyo akapooza sehemu ya chini ya mguu wake. Hivi sasa anaendelea na matibabu na hali yake ni nzuri.Uchunguzi uliofanywa na Kituo cha Marekani cha Kudhibiti na Kuzuia magonjwa, CDC ukaunganisha virusi hivyo na aina ya ile iliyobainika kwenye mazingira huko Gaza mwezi Juni mwaka huu.Sasa WHO imethibitisha kuwa ni polio ambapo Mkurugenzi Mkuu wa UNRWA Philippe Lazzarini kupitia mtandao wa X amesema “inasikitisha sana kwamba mtoto huyo amepooza kutokana na Polio. Polio haitotofautisha kati ya watoto wa Palestina na Israeli. Kuchelewecha sitisho la mapigano kwa misingi ya kiutu kutaongeza hatari ya ugonjwa huo kusambaa zaidi kwa watoto.”Awamu mbili za utoaji chanjo zimepangwa kuanza wiki zijazo na UNRWA imesema wataalamu wake wa afya na kupitia kliniki zake tembezi watasaidia usambazaji kwa ushirikiano na WHO na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.
  continue reading

101 episodes

Semua episode

×
 
Loading …

Welcome to Player FM!

Player FM is scanning the web for high-quality podcasts for you to enjoy right now. It's the best podcast app and works on Android, iPhone, and the web. Signup to sync subscriptions across devices.

 

Quick Reference Guide