Artwork

Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Player FM - Podcast App
Go offline with the Player FM app!

UN: Hali inaendelea kuwa kizungumkuti Gaza mashambulizi yakishika kasi

1:57
 
Share
 

Manage episode 429363242 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Hali ya kibinadamu inaendelea kuwa mbaya Gaza huku leo mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa yakiripoti kuendelea kwa mashambulizi yanayokatili maisha ya watu na kuathiri miundombinu ya raia kuanzia kwenye shule hadi vituo vya afya huku maelfu ya watu wakiendelea kukabiliwa na ukosefu wa huduma za msingi ikiwemo afya, makazi, maji na chakula kadri vita vinavyoendelea. Asante Leah nikianza na shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO ambalo leo limeendelea kusihi pande zinazozozana kwenye Ukanda wa Gaza kuheshimu sheria za kimataifa na kulinda vituo vya afya na wahudumu wa afya linasema tangu Oktoba 7 mwaka jana mzozo huu mpya ulipozuka limeorodhesha mashambulizi zaidi ya 1000 kwenye vituo vya afya katika eneo hilo linalokaliwa la Palestina.Hivyo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X limesema “Tunatoa ombi la ulinzi wa wahudumu wa afya na vituo vya afya kwa ajili ya fursa za kuweza kutoa msaada wa kibinadamu na mapigano lazima yakome mara moja.”Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA likiunga mkono usitishwaji wa mapigano mara moja kwa minajili ya kibinadamu limesema Watoto wa Ukanda wa Gaza wameporwa utoto wao na mustakbali wao, elimu imegeuka ndoto na madhila ya kiafya ni tishio lingine.Philippe Lazzarini Kamishina Mkuu wa UNRWA ameandika kwenye ukurasa wake wa X kwamba “Karibu kila siku kuna mashambulizi dhidi ya vituo vya elimu. Takribani shule 8 zimeshambuliwa katika siku 10 zilizopita zikiwemo shule 6 za UNRWA. Vita vimewapora wasichana na wavulana wa Gaza utoto wao na elimu yao.”Ameongeza kuwa changamoto za afya ni mtihani mwingine unaotishia mustakbali wa watoto wa Gaza akimtolea mfano mvulana wa umri wa miaka minne akisema “ Mvulana huyu anaugua magonjwa ya ngozi kutokana na hali mbaya ya familia yake, wakilala katika mahema yaliyoezekwa kwa karatasi za plastiki bila kupata vifaa vya usafi au maji safi ya kutosha hii ni hatari kubwa. Timu zetu za UNRWA zinatoa dawa, lakini bila ya hali kuboreka, maambukizi ya magonjwa yanarudi tena”.Amesisitiza kwamba ili madhila yote haya yaishe ni lazima vita vikome mara moja.
  continue reading

100 episodes

Artwork
iconShare
 
Manage episode 429363242 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Hali ya kibinadamu inaendelea kuwa mbaya Gaza huku leo mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa yakiripoti kuendelea kwa mashambulizi yanayokatili maisha ya watu na kuathiri miundombinu ya raia kuanzia kwenye shule hadi vituo vya afya huku maelfu ya watu wakiendelea kukabiliwa na ukosefu wa huduma za msingi ikiwemo afya, makazi, maji na chakula kadri vita vinavyoendelea. Asante Leah nikianza na shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO ambalo leo limeendelea kusihi pande zinazozozana kwenye Ukanda wa Gaza kuheshimu sheria za kimataifa na kulinda vituo vya afya na wahudumu wa afya linasema tangu Oktoba 7 mwaka jana mzozo huu mpya ulipozuka limeorodhesha mashambulizi zaidi ya 1000 kwenye vituo vya afya katika eneo hilo linalokaliwa la Palestina.Hivyo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X limesema “Tunatoa ombi la ulinzi wa wahudumu wa afya na vituo vya afya kwa ajili ya fursa za kuweza kutoa msaada wa kibinadamu na mapigano lazima yakome mara moja.”Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA likiunga mkono usitishwaji wa mapigano mara moja kwa minajili ya kibinadamu limesema Watoto wa Ukanda wa Gaza wameporwa utoto wao na mustakbali wao, elimu imegeuka ndoto na madhila ya kiafya ni tishio lingine.Philippe Lazzarini Kamishina Mkuu wa UNRWA ameandika kwenye ukurasa wake wa X kwamba “Karibu kila siku kuna mashambulizi dhidi ya vituo vya elimu. Takribani shule 8 zimeshambuliwa katika siku 10 zilizopita zikiwemo shule 6 za UNRWA. Vita vimewapora wasichana na wavulana wa Gaza utoto wao na elimu yao.”Ameongeza kuwa changamoto za afya ni mtihani mwingine unaotishia mustakbali wa watoto wa Gaza akimtolea mfano mvulana wa umri wa miaka minne akisema “ Mvulana huyu anaugua magonjwa ya ngozi kutokana na hali mbaya ya familia yake, wakilala katika mahema yaliyoezekwa kwa karatasi za plastiki bila kupata vifaa vya usafi au maji safi ya kutosha hii ni hatari kubwa. Timu zetu za UNRWA zinatoa dawa, lakini bila ya hali kuboreka, maambukizi ya magonjwa yanarudi tena”.Amesisitiza kwamba ili madhila yote haya yaishe ni lazima vita vikome mara moja.
  continue reading

100 episodes

Усі епізоди

×
 
Loading …

Welcome to Player FM!

Player FM is scanning the web for high-quality podcasts for you to enjoy right now. It's the best podcast app and works on Android, iPhone, and the web. Signup to sync subscriptions across devices.

 

Quick Reference Guide