Artwork

Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Player FM - Podcast App
Go offline with the Player FM app!

Tanzania, Kenya na Uganda zasonga mbele kuzuia maambukizi ya UKIMWI kwa watoto- UNAIDS

1:59
 
Share
 

Manage episode 430207734 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Ripoti mpya iliyotolewa leo kwa pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na ukimwi UNAIDS na muungano wa kimataifa wa kutokomeza ukimwi unaojumuisha mashirika mbalimbali, inaonyesha kwamba dunia iko katika wakati muhimu wa kubaini endapo viongozi wa dunia watatimiza ahadi zao za kumaliza janga la ukimwi kama tishio la afya ya umma ifikapo mwaka 2030. Ripoti hiyo, iliyotolewa mjini Geneva na Munich inasisitiza uharaka wa kuchukua hatua kwani ukimwi uko njiapanda na inatanabaiisha, takwimu mpya na tafiti zinazoonyesha kwamba maamuzi na uchaguzi wa sera vinahitajika sasa.Inasema utoaji wa haraka wa huduma za VVU pekee ndio utakaotimiza ahadi ya kukomesha UKIMWI kwa watoto ifikapo 2030.Ripoti hiyo”Kubadili maono kuwa hali halisi” inaonyesha kwamba janga la Ukimwi linaweza kumalizika ifikapo 2030, endapo viongozi wa dunia wataongeza rasilimali na kulinda haki za binadamu hivi sasa.Kwani inaonyesha kuwa programu maalum zinazolenga maambukizi ya VVU zimesaidia kuepusha maambukizi milioni 4 miongoni mwa watoto wenye umri wa miaka 0-14 tangu mwaka 2000.Ulimwenguni kote, maambukizi mapya ya VVU miongoni mwa watoto wenye umri wa miaka 0-14 yamepungua kwa asilimia 38 tangu mwaka 2015 na vifo vimepungua kwa asilimia 43.Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS, Winnie Byanyima amesema"Ninapongeza maendeleo ambayo mataifa mengi yanapata katika kusambaza huduma za VVU ili kuwapa afya bora wanawake vijana na kuwalinda watoto wachanga na watoto wengine dhidi ya VVU. Kwa dawa na sayansi zilizopo leo, tunaweza kuhakikisha kuwa watoto wote wanazaliwa na kuishi bila VVU, na kwamba watoto wote wanaoishi na VVU wanapata huduma na kusalia kwenye matibabu. Huduma za matibabu na kinga lazima ziongezeke mara moja ili kuhakikisha kuwa zinawafikia watoto wote kila mahali. “Ameongeza kuwa Hatuwezi kupumzika kwani kifo cha mtoto yeyote kutokana na sababu zinazohusiana na UKIMWI sio tu janga, lakini pia hasira. Ninakotoka, watoto wote ni watoto wetu. Ulimwengu unaweza na lazima utimize ahadi yake ya kukomesha UKIMWI kwa watoto ifikapo 2030.”Miongoni mwa nchi 12 za muungano wa kimataifa wa kutokomeza ukimwi, kadhaa zimefanikisha upatikanaji wa matibabu ya kudumu ya dawa za kuongeza mud awa kuishi miongoni mwa wanawake wajawazito na wanaonyonyesha wanaoishi na VVU, huku Uganda ikikaribia asilimia 100, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 98, na Afrika Kusini kwa asilimia 97, Msumbiji imefikia asilimia 90, Zambia asilimia 90, Angola na Kenya kwa asilimia 89, Zimbabwe kwa asilimia 88, na Cote d'Ivoire kwa asilimia 84.
  continue reading

100 episodes

Artwork
iconShare
 
Manage episode 430207734 series 2027789
Content provided by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. All podcast content including episodes, graphics, and podcast descriptions are uploaded and provided directly by UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations or their podcast platform partner. If you believe someone is using your copyrighted work without your permission, you can follow the process outlined here https://player.fm/legal.
Ripoti mpya iliyotolewa leo kwa pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na ukimwi UNAIDS na muungano wa kimataifa wa kutokomeza ukimwi unaojumuisha mashirika mbalimbali, inaonyesha kwamba dunia iko katika wakati muhimu wa kubaini endapo viongozi wa dunia watatimiza ahadi zao za kumaliza janga la ukimwi kama tishio la afya ya umma ifikapo mwaka 2030. Ripoti hiyo, iliyotolewa mjini Geneva na Munich inasisitiza uharaka wa kuchukua hatua kwani ukimwi uko njiapanda na inatanabaiisha, takwimu mpya na tafiti zinazoonyesha kwamba maamuzi na uchaguzi wa sera vinahitajika sasa.Inasema utoaji wa haraka wa huduma za VVU pekee ndio utakaotimiza ahadi ya kukomesha UKIMWI kwa watoto ifikapo 2030.Ripoti hiyo”Kubadili maono kuwa hali halisi” inaonyesha kwamba janga la Ukimwi linaweza kumalizika ifikapo 2030, endapo viongozi wa dunia wataongeza rasilimali na kulinda haki za binadamu hivi sasa.Kwani inaonyesha kuwa programu maalum zinazolenga maambukizi ya VVU zimesaidia kuepusha maambukizi milioni 4 miongoni mwa watoto wenye umri wa miaka 0-14 tangu mwaka 2000.Ulimwenguni kote, maambukizi mapya ya VVU miongoni mwa watoto wenye umri wa miaka 0-14 yamepungua kwa asilimia 38 tangu mwaka 2015 na vifo vimepungua kwa asilimia 43.Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS, Winnie Byanyima amesema"Ninapongeza maendeleo ambayo mataifa mengi yanapata katika kusambaza huduma za VVU ili kuwapa afya bora wanawake vijana na kuwalinda watoto wachanga na watoto wengine dhidi ya VVU. Kwa dawa na sayansi zilizopo leo, tunaweza kuhakikisha kuwa watoto wote wanazaliwa na kuishi bila VVU, na kwamba watoto wote wanaoishi na VVU wanapata huduma na kusalia kwenye matibabu. Huduma za matibabu na kinga lazima ziongezeke mara moja ili kuhakikisha kuwa zinawafikia watoto wote kila mahali. “Ameongeza kuwa Hatuwezi kupumzika kwani kifo cha mtoto yeyote kutokana na sababu zinazohusiana na UKIMWI sio tu janga, lakini pia hasira. Ninakotoka, watoto wote ni watoto wetu. Ulimwengu unaweza na lazima utimize ahadi yake ya kukomesha UKIMWI kwa watoto ifikapo 2030.”Miongoni mwa nchi 12 za muungano wa kimataifa wa kutokomeza ukimwi, kadhaa zimefanikisha upatikanaji wa matibabu ya kudumu ya dawa za kuongeza mud awa kuishi miongoni mwa wanawake wajawazito na wanaonyonyesha wanaoishi na VVU, huku Uganda ikikaribia asilimia 100, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 98, na Afrika Kusini kwa asilimia 97, Msumbiji imefikia asilimia 90, Zambia asilimia 90, Angola na Kenya kwa asilimia 89, Zimbabwe kwa asilimia 88, na Cote d'Ivoire kwa asilimia 84.
  continue reading

100 episodes

All episodes

×
 
Loading …

Welcome to Player FM!

Player FM is scanning the web for high-quality podcasts for you to enjoy right now. It's the best podcast app and works on Android, iPhone, and the web. Signup to sync subscriptions across devices.

 

Quick Reference Guide